Hapa na Pale pamekuwa na minong'ono kwamba baadhi ya waishio suria wamekuwa wakijificha kwenye Vyama vya Kitume kupoza maumivu ya dhamiri zao kwa maisha ya uzinzi maana aishie na mwanamke au mwanamume bila kufunga ndoa halali Kanisani azini na hushauriwa tu kuikimbia zinaa (1Kor 6:18) maana azinie na Mwanamke Maandiko Matakatifu husema hana akili kabisa (Mithali 6:32-34) kwa sababu hiyo hushauriwa kurekebisha au basi kutafuta kibali kutoka kwa Mungu (Mithali 18:22) kwani ajipatiaye Mke halali hujipatia Kibali kutoka kwa Mungu mwenyewe. Mwito wa Askofu Mkuu Isaac Amani wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha wa kutopokewa kwa waishio Suria, yaani washio mwanamke na mwanamume pamoja kama mke na mume bila Kibali cha Mungu hawaruhusiwi kujiunga au hata kupokewa kwenye Chama chochote cha Kitume hadi hapo watakaporekebisha hayo maisha yao kama Mwanampotevu, wakaamua kumrudia Mungu kwa Kufunga Ndoa ndipo wataruhusiwa kujiunga na chama chochote wapendacho. Hayo ameyasema kwenye Kongamano la Familia lililoendeshwa na Wanautume wa Familia ya Nyumba Aminifu Kanisa Kuu la Mt Theresa Arusha kuelekea Kilele cha Jubilei ya Miaka 60 ya Jimbo Kuu Arusha.
- Күн бұрын
ASKOFU MKUU ISAAC AMANI WA JIMBO KUU ARUSHA APIGA STOP SURIA KUJIUNGA VYAMA KITUME HADI WAREKEBISHE
- Рет қаралды 1,525
Пікірлер: 3