Watu wawili wa familia moja Mwihidini Mangunga (69), mkazi wa Kijiji cha Likaha kwa kunyongwa na shati shingoni na kujeruhiwa kwa kukatwa kichwani na kitu chenye incha kali kisha kufunikwa na majani makavu, huku mtoto wake Ramadhan Mwihidini (10), mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Kitomanga ameuawa kwa kunyongwa shingoni na waya wa umeme wa solar kisha kutupwa kwenye vichaka.
Matukio hayo mawili kwa pamoja yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, ACP, John Imori.
Kamanda wa polisi mkoa wa lindi, amesema kuwa marehemu hao hawakuonekana nyumbani kuanzia siku ya juni 12,2024 siku nzima ndipo ilipofika asubuhi ya juni 13,2024 majira ya saa 07:00 wananchi waliamua kufanya msako kwa kuzungukia maeneo ya jirani na nyumba ya familia hiyo kuwatafuta ndipo walipokuta miili ya marehemu hao shambani kwa marehemu.
Негізгі бет BABA NA MTOTO WAUAWA KWA KUNYONGWA NA KUTUPWA KICHAKANI-LINDI
Пікірлер