Mradi huo utaanza katikati ya jiji, kutoka kituo cha mabasi cha Mnazi Mmoja barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Barabara ya Bagamoyo hadi Tegeta na Boko
Aidha serikali imetoa shilingi bilioni 570.6/- ($248.1m) kwa ajili ya kutekeleza BRT Awamu ya tatu na nne ambapo awamu ya III inahusisha ujenzi wa barabara ya kilomita 23.6 kutoka Gongolamboto hadi katikati ya jiji, kando ya Barabara ya Nyerere, na sehemu ya Barabara ya Uhuru kutoka Tazara hadi Kariakoo-Gerezani
Serikali ya Tanzania kupitia Tanroads leo 30 Juni 2023 ilisaini Mikata Minne ya ujenzi wa miundombinu ya Usafiri wa haraka wa Mabasi (BRT) awamu ya nne.
Inaanza kujenga barabara ya Magari yaendayo haraka kutoka Katikati ya Mji (Maktaba) hadi Tegeta, ambayo itajengwa na Wakandarasi wawili. Mmoja kutoka Maktaba kadi Morocco na mwingine kutoka Morocco hadi Tegeta ikiwemo ujenzi Madaraja.
Pia Serikali imesaini Mkataba wa upanuzi wa barabara ya Morogoro kutoka Ubungo hadi Kimara kuwa ya njia nane kutoka Njia sita za sasa. #tanzania #tegeta ##Mbezibeach #daressalaam
Негізгі бет Barabara ya Tegeta Ujenzi wa mwendokas / Kivukoni-Tegeta-Boko 🇹🇿
Пікірлер: 10