Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba amepokea Boti ya kisasa ya Mwendokasi kutoka Kampuni ya Zan Fast Ferries kwa ajili ya Usafirishaji wa abiria itakuyokuwa ikifanya safari kutoka Tanga kuelekea Unguja na Pemba ikiwa ni mara ya kwanza katika Historia ya mkoa huo kupokea Boti aina hiyo.
Waziri Kindamba amepokea Boti hiyo katika Bandari ya Tanga mara baada ya kuwasili kutokea Visiwani Zanzibar ambapo amesema kuwasili kwa boti hiyo ya kisasa ni kutokana na mazingira rafiki ya uwekezaji wa biashara ambayo yanafanywa na kusimamiwa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Zanzibar Mhe.Dkt Hussein Mwinyi.
Amesema boti hiyo itakuwa ikifanya safari zake za kutoka Tanga kwenda Pemba na Pemba kwenda Unguja kwa siku za Jumamosi,jumatatu, na jumatano
Aidha Kindamba Amesema uwekezaji uliofanywa na Kampuni hiyo si chini ya Dollar Milioni 10 hadi 15, ambapo ameipongeza kampuni ya Zan Fast Ferries kwa uwekezaji huo katika Sekta ya Usafirishaji mkoani Tanga ambapo amewahakikishia Ulinzi na Usalama wa uwekezaji huo
Негізгі бет BOTI MPYA YAKISASA YAWASILI TANGA - SAFARI TANGA,PEMBA NA UNGUJA
Пікірлер: 28