Hakimu Monica Kivuti aliyeuwawa akiongoza kikao cha mahakama hapa Nairobi amezikwa nyumbani kwao eneo la Yatta kaunti ya Machakos
Akiwaongoza maafisa wa idara ya mahakama kumpa buriani, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu ametaka kukomeshwa kwa mauwaji ya maafisa wa idara ya mahakama. Mwilu akidai kumekuwa na majaribio mengi ya kuwaangamiza maafisa wa mahakama. Wengine waliozungumza pia walitaka usalama zaidi katika mahakama kote nchini. Hakimu Kivuti alifariki kutokana na majeraha ya risasi aliyopigwa na afisa wa polisi alipokuwa akiongoza kesi katika mahakama ya Makadara.
Негізгі бет Hakimu Monica Kivuti amezikwa nyumbani kwake Yatta kaunti ya Machakos
Пікірлер: 3