Mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajabu Abdallah amewataka wananchi wa Pangani kuwafichua watu wanaojihusisha na biashara za magendo pamoja na kusafirisha dawa za kulevya kupitia bandari ya Kipumbwi ambayo serikali iliirasimisha bandari hii kwa lengo la kuingiza mapato na kuwarahisishia wananchi kufanya biashara halali wa Pangani Mkoani Tanga na visiwa vya Zanzibari kufanya biashara zao.
MCC Rajabu ameyasema hayo wakati alipotembelea kituo cha Polisi cha Kipumbwi wilayani Pangani na kukabidhi shilingi Milion 5 kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi katika kituo hicho.
Aidha Mjumbe huyo wa kamati kuu ya CCM Taifa akawataka viongozi kuacha kuwatetea wananchi wanaojishughulisha na uhalifu.
Негізгі бет HATUTOWAVUMILIA WANAOFANYA BIASHARA YA MAGENDO NA DAWA ZA KULEVYA.
Пікірлер