TGNP ina furaha kubwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa mradi unaofadhiliwa na UNFPA, wa kugawa taulo za kike/pedi zinazoweza kutumika tena, kwa wasichana wanaotoka kwenye mazingira magumu katika shule mbalimbali mkoani Shinyanga.
Mradi huu ni sehemu ya mkakati endelevu kati ya serikali na wadau kuhakikisha hedhi salama, na kupunguza gharama za pedi kila mwezi kwa wasichana waliopo kwenye mazingira magumu, na hivyo kupunguza idadi ya wasichana wanaorubuniwa na kupata mimba, ndoa za utotoni, na kuacha shule kabisa.
Katika kusimamia mradi huu TGNP imetumia pia nafasi hii kuendelea kuishauri na kuihamasisha serikali kuweka kipaumbele katika utengwaji wa bajeti maalumu kwaajili ya ununuzi na utolewaji wa pedi mashuleni, ikiwa pia ni utekelezaji wa bajeti yenye mrengo wa kijinsia kwa maendeleo endelevu.
Негізгі бет HEDHI SALAMA KWA WOTE
Пікірлер