SHALOM WATU WA MUNGU.
Huu ni wimbo kutoka KWAYA YA VIJANA KKKT MTAA WA KULANGWA uitwao HERI.
Wimbo huu ulio kwenye mahadhi ya morden taarabu. Maneno ya wimbo huu yametoka katika kitabu cha Zaburi 119:1.
WIMBO UNAELEZEA WATU WA AINA TATU.
Aina ya kwanza ni watu walio zishika sheria za Mungu na maagizo yake kuwa wamebarikiwa lakini aina nyingine ya watu ni ambao hawajazishika sheria za Mungu wanakumbushwa kuwa kuna siku itafika, kuna wakati utafika utatoa hesabu kwa matendo yako mabaya.
Aina ya tatu ni yule aliye gundua siri baada ya kuteseka na kusumbuka kwa muda mwingi lakini baada ya kugundua siri ni kuwa na YESU mateso yote,shida na magonjwa yote yalikwisha.
Tunajua wimbo huu umezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza na kuhoji kuwa TAARABU IMEHAMIA MAKANISANI?
lakini Jibu letu ni HAPANA tena HAPANA KUBWA.
Lengo letu ni kuwatafuta watu mbalimbali ambao bado awajapata neema ya kumjua Huyu YESU tunae mtumikia sisi KWAYA YA VIJANA KKKT KULANGWA.
Lakini pia kama dunia inawaona waimba taarabu kama watu waliopotea na ni wenye dhambi.
Basi sisi kama vijana tumeamua kuwapenda nakuwasogezea injilii kupitia mahadhi ya wanachokipenda tukumbuke pia YESU akuja duniani kwaajili ya watakatifu bali kutafuta walio potea na wenye dhambi.
Mwisho tunaomba radhi kwa wale wote tulio wakwaza kwa aina hii ya injili yetu, imani yetu ni kuwa kama tulikuwa wenye dhambi na tukaokolewa, basi hatuwezi kamwe kuacha kuwafuata wenye dhambi na kuwaambia waje wamjue huyu YESU mwenye huruma anayewapenda wote bila kujali ni wenye dhambi au laah.
N:B UNAIKATAA TAARABU HUKU KANISANI KWAKO UNAIMBA RAGAE, MAKHIRIKHIRI, SEBENE, LUMBA, ZOUK, CHAKACHA
Sisi kama vijana tunauliza mnajua zimetoka wapi na asili yake ni wapi?
Ila kama hujui basi acha YESU ahubiriwe kwa namna zote na kwa mataifa yote.
MARKO 13:10
"NA SHARTI INJILI IHUBIRIWE KWANZA KATIKA MATAIFA YOTE"
KWAYA YA VIJANA KKKT MTAA WA KULANGWA.
#gospel #taarabu
Негізгі бет HERI (Official Video) - KWAYA YA VIJANA KKKT KULANGWA.
Пікірлер: 12