KENYA NI TAIFA LETU
Wananchi wazalendo wa taifa letu Kenya heko
kwetu kwa kudumisha amani, umoja na
upendo kila wakati, tuungane kwa pamoja
tulijenge taifa letu [sisi wazalendo] Mungu
atupenda sote tulijenge taifa letu..
Kenya ni taifa letu lenye amani, upendo pia
umoja twafurahia, [Ewe Mungu Mungu Baba,
tunakuomba uilinde nchi yetu milele na
milele.x2]
1. Wananchi wazalendo, tudumishe umoja
wetu, palipo na ‘pendo kweli Mungu yupo.
2. Tuwape maskini, wazee pia na wajane, na
wote wanyonge tusiwanyanyase,
3. Raisi na mabalozi, mawaziri na wabunge
nasi watu wote tuwe waaminifu.
4. Tuheshimu sheria, na viongozi wetu wote,
hilo ni agizo toka kwake Mungu.
Негізгі бет KENYA TAIFA - ST. CECILIA CHOIR SHAURI MOYO NAIROBI
Пікірлер: 30