#soyabeans #soyabean #soya #kilimochasoya #soyamilk #kilimo #mazingira #kilimobora #kilimochakisasa #kilimobora #tanzania
#china #mitanotena #soya #magufuli #shambadarasa #mbegu #sua
#subscribe #2021
Mazingira yanayofaa kwa uzalishaji
➡️Soya huhitaji mvua ya kutosha ya wastani wa
milimita 350 hadi 1,500 kwa mwaka
inayonyesha katika mtawanyiko mzuri au
umwagiliaji maji ili kuhakikisha upatikanaji wa
unyevu wa kutosha kuanzia upandaji hadi
inapotoa maua na matunda. Uvunaji ni
muhimu ufanyike wakati hakuna mvua ili
kuruhusu soya kukauka vizuri na kutunza
ubora wake.
➡️Soya kama yalivyo mazao mengine, huhitaji
udongo wenye rutuba na usiotuamisha maji.
Hivyo kama shamba halina rutuba ya kutosha,
ni muhimu kutumia mbolea. Mbolea za
viwandani zinazoweza kutumika ni aina ya
DAP na TSP (wastani wa kilo 80 hadi 100
kwa hekta moja) kwa ajili ya kupandia na
(wastani wa kilo 60 hadi 80 kwa hekta) za
mbolea ya kukuzia kama CAN. Ni muhimu
kupata ushauri wa kitaalam juu ya rutuba ya
udongo kabla ya kuamua kutumia mbolea.
Uzalishaji ⬇️
Ni muhimu kuzingatia misimu ya mvua ya
mahali husika na aina ya soya inayofaa ili
kuruhusu soya kukomaa wakati hakuna mvua
na hivyo kuhifadhi ubora wake.
1. Shamba liandaliwe kwa kuondoa magugu
na kutifuliwa. Soya inaweza kupandwa katika
matuta au katika mistari.
2. Nafasi inayofaa katika kupanda soya ni
Sm.5 hadi 10 kati ya mashina na Sm. 45 hadi
60 kati ya mstari na mstari kutegemea aina ya
soya na rutuba ya udongo.
3. Kila shimo lipandwe mbegu moja katika
kina cha sentimita 2 hadi tano na kufukiwa
vizuri kwa udongo.
4. Palizi ifanyike kuondoa magugu, ikiwa soya
itastawi na kufunika udongo vizuri inaweza
kupunguza uhitaji wa kupalilia zaidi.
5. Soya huchukua wastani wa miezi mitatu
hadi saba kukomaa kutegemea na aina,
mahali ilikopandwa na utunzaji wa shamba.
Негізгі бет Kilimo Cha Zao La SOYA | Mazingira yafaayo KULIMA | MBOLEA | DAWA | FAIDA za Zao Hilo.
Пікірлер: 16