WAMILIKI WA MAGARI YA SHULE WASIOPELEKA MAGARI YAO KUKAGULIWA KUKIONA
Jeshi la polisi mkoa wa Mwanza limewaonya wamiliki wa magari ya shule wasiopeleka magari yao kukaguliwa na kusema halitasita kuwachukuli hatua za kisheria
Kauli hiyo imetolewa leo na kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza DCP Wilbroad Mutafungwa wakati akifungua rasmi zoezi la ukaguzi wa magari ya shule katika mkoa huo
lililofanyika katika uwanja wa stendi ya mabasi nyamhongoro na kuambatana na na utolewaji wa Elimu kwa madereva pamoja na ukaguzi wa leseni
Nae Mkuu wa kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Mwanza (RTO) mrakibu wa polisi (SP ) Sunday ibrahim amesema zaidi ya magari 50 yamefika kukaguliwa na amewataka wale ambao awajapekeka magari yao kukaguliwa wayapeleka kabla awajawajibishwa kisheria .
Kwa upande wake Baraka Daudi ambaye ni dereva wa gari ya shule ya Musabe amepongeza jeshi la polisi Kwa kufanya zoezi Hilo la ukaguzi wa magari pamoja Na ukaguzi wa leseni
Zaidi ya magari 50 Hadi Sasa yamekaguliwa huku zoezi la ukaguzi likitarajiwa kuhitimishwa ijumaa ya wiki hii
Негізгі бет 🛑LIVE :ZAIDI YA MAGARI 50 YA SHULE YAKAGULIWA MWANZA.
Пікірлер