Maiti iliyozikwa kimakosa na familia moja katika eneo la Khwisero kaunti ya Kakamega imefukuliwa na kurejeshwa kwenye hifadhi ya maiti katika hospitali ya Yala ilikokuwa imetolewa. Wakati huo huo, wanakijiji walianza matambiko ya kuitakasa familia hiyo kulingana na tamaduni ya jamii ya Luhya. Wakati wote maiti ikifukuliwa, Justus Olukoye aliyedhaniwa kafariki alikuwa amefichwa na anatarajiwa kukaribishwa kwenye boma lao siku ya Ijumaa baada ya kufanyiwa tambiko pia.
Негізгі бет Maiti Iliyozikwa Kakamega Yafukuliwa
Пікірлер: 94