Mashindano ya mbio za baisikeli yaliyopewa jina "Live Free Race" yalifanyika jijini Nairobi, yakiandaliwa kwa ushirikiano kati ya Kampuni ya Bima ya Jubilee na Royal Media Services. Katika makala haya ya nne, waandalizi walilenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuimarisha afya kupitia mazoezi.Zaidi ya watu 3,000 walijitokeza kushiriki mbio hizo za baisikeli zilizofanyika siku ya Jumapili, na walipata fursa ya kipekee ya kutangamana na watangazaji maarufu wa Hot 96, Jeff Koinange na Patrick Igunza, ambao walisisitiza umuhimu wa kufanya mazoezi mara kwa mara kama njia ya kuimarisha afya.Miongoni mwa walioshiriki walikuwa ni makundi tofauti, yakiwemo waendesha baisikeli wenye changamoto za kusikia, ambao walionyesha azma yao ya kujumuika na jamii katika kuimarisha afya.
Негізгі бет Mashindano ya "Live Free Race" yafanyika jijini Nairobi
Пікірлер