Aliyekuwa katibu mkuu wa Chama cha walimu Tanzania (CWT) Japhet Maganga na wenzake tisa bado wanashikiliwa na jeshi la polisi Mkoani Dodoma tangu walipokamatwa Februari 16, mwaka huu kwa kile kinachodaiwa kufanya fujo kwenye mkutano wa baraza kuu la chama hicho Jijini Dodoma.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Martin Otieno amesema bado wanawashikilia watu hao na watafikishwa mahakamani taratibu za upelelezi zitakapokamilika.
Maganga na wenzake tisa walikamatwa siku ya Alhamisi kwenye mkutano wa baraza kuu la CWT kwa madai ya kufanya fujo kwenye mkutano huo baada ya Maganga kudai kuwa hana imani na mwenyekiti wake (Leah Ulaya) hivyo aliomba makamu mwenyekiti aongoze kikao hicho.
Mmoja wa wajumbe wa baraza la Taifa la CWT, Emmanuel Kihako amesema wamejitahidi kuwawekea dhamana watuhumiwa 10 wanachama wa CWT waliokamatwa lakini hawajafanikiwa mpaka Sasa.
Негізгі бет Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CWT aonya kuhusu Mwalimu Maganga aibua ya Oluoch
Пікірлер: 7