Muigizaji nguli wa filamu kutoka nchini Afrika Kusini, #ConnieChiume, atatoa mafunzo maalumu ya filamu (Masterclass) jijini Dar es Salaam, Jumamosi ya April 24. Chiume ambaye ameigiza kwenye filamu nyingi kubwa ikiwemo Black Panther ya Marvel, analetwa nchini na taasisi ya #RefocusAfrica.
Akizungumza na SnS kuhusiana na ujio wa Chiume, Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Refocus Africa, Sunshine Silas, amesema hiyo ni fursa kwa waandaji na waigizaji wa filamu kujifunza mbinu muhimu za kuipeleka kimataifa tasnia ya filamu nchini Tanzania.
“Wewe ni muigizaji au mtayarishaji? Au labda ni muigizaji mchanga na hujapata nafasi bado, hujulikani lakini unapenda uigizaji au unaona kuwa una kipaji, Connie Chiume anasema ‘kama unataka kuwa nyota nataka kukusaidia uwe nyota,” amesema Sunshine.
Sunshine ameeleza kuwa baada ya mafunzo hayo washiriki pia watapewa vyeti maalum. “Ni muhimu kwakuwa tunaenda kuwa na programu za mabadilishano ambapo wanafunzi katika shule yetu ya filamu wataweza kwenda kumaliza programu zao kwenye shule yake ya filamu. Sababu ni kwamba tunataka kuwapa exposure kwenye tasnia zingine,” ameongeza.
Kwa upande wa namna ya kushiriki, Sunshine amesema gharama ya kujisali ni shilingi 50,000 tu. Amedai kuwa wameamua kuweka kiwango hicho ili mtu yeyote aweze kiumudu.
Kwa anayetaka kushiriki anaweza kuwasiliana nao kwa WhatsApp au kupiga simu kwa kutumia namba hizi: 0719828650 au 0782119441 na wanaweza kutuma hela ya usajili kwa kutumia namba ya Airtel Money 0683077527.
Негізгі бет Muigizaji wa Black Panther, Connie Chiume kutoa mafunzo ya filamu Dar, April 24
Пікірлер: 9