Mzee mmoja wa umri wa miaka 60 amewashangaza wanakijiji cha Mugono eneo la Kiharu kaunti ya Muran’ga kwa kubadilisha kitanda chake kuwa nyumba anamoishi katikati ya shamba lake dogo kutokana na kile kinachotajwa kuwa ni uchochole wa hali ya juu. Kamau Mwangi amekuwa akiishi katika hali hiyo kwa miaka 6 sasa baada ya kuuza shamba lake la ekari mmoja alilorithi kutoka kwa wazazi wake kwa lengo la kununua matatu ya kufanyia biashara ya uchukuzi lakini badala yake akazitumia pesa zote kwenye ulevi. Mzee huyo anaomba wasamaria wema kumsaidia angalau abadilishe mkondo wa maisha yake.
Негізгі бет Mzee Aliuza Shamba Na Kunywa Pombe Na Pesa
Пікірлер: 162