Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko amemtaka mmiliki wa leseni ya uchimbaji dhahabu katika machimbo ya Msege yaliyopo Tarime mkoani Mara, kuingia makubaliano ya kufanya kazi pamoja na wachimbaji wadogo waliowekeza mitaji yao kwenye machimbo hayo.
Maamuzi hayo ni matokeo ya ziara aliyoifanya jumatano iliyopita Septemba 19, 2018 kwenye machimbo hayo ambapo alimuonya mmiliki huyo Mwita Chacha Wambura (Dochi), kuheshimu maamuzi yaliyoafikiwa kwani amekuwa akikwepa kusaini makubaliano yaliyopo ambapo anapaswa kupata asilimia 40 ya mauzo ya dhahabu katika machimbo hayo huku wachimbaji wadogo wakipata asilimia 60.
Негізгі бет Naibu Waziri Doto Biteko atatua mgogoro wa madini Tarime
Пікірлер