Leo tunasoma kitabu cha Luka sura ya kumi na tano, na tunaenda kufanya maombi ya toba na urejesho. Moja kati ya madhara ya kiroho yanayotokana na dhambi na uovu, ni kupoteza vitu tunavyotakiwa kuwa navyo.
Na njia pekee ya kurudisha ni kuomba toba na rehema kwa Mungu. Na ndicho kitu tunachoenda kukifanya siku ya leo kupitia maombi haya. Mungu anaenda kukusaidia kurejesha mambo yaliyopotea ambayo Mungu anataka uwe nayo.
Nakuombea kupitia maombi haya ukamuone Mungu akikupigania na kukushindia. Damu ya YESU inene mema kwa ajili yako na ukauone uaminifu wa Mungu kwenye kila jambo linalogusa maisha yako. Mungu akupe nyakati zenye kuburudishwa na ukaishi kwenye uheri na utoshelevu. Amen
Isaac Javan
+255 745 76 45 72
Негізгі бет NENO LA SIKU | Luka 15 | Maombi Ya Toba Na Urejesho
Пікірлер: 39