144-Ni Wako Bwana
I Am Thine O Lord (SDAH306)
Doh ni A♭
Ni wako, Bwana, ninasikia Unaponena nami;
Lakini, kweli, nataka kwako Nizidi kusongea;
CHORUS
Bwana vuta, (vuta) nije nisongee
Sana kwako mtini,
Bwana, vuta, vuta, nije nisongee
Pa damu ya thamani.
Niweke sasa nikatumike Kwa nguvu za neema;
Utayopenda nami nipende Nizidi kukwandama.
Nina furaha tele kila saa Nizungumzapo nawe;
Ninanena kama kwa rafiki Nikipiga magoti.
Негізгі бет NI WAKO BWANA (VIDEO LYRICS) wimbo no.144
Пікірлер: 10