Mwaka 2009 Wafugaji wa Jamii ya Kimaasai waishio katika tarafa ya Ngorongoro mkoani Arusha walinyimwa fursa ya kulima baada ya kukatazwa na Serikali kufanya hivyo kupitia baadhi ya Kanuni za Uhifadhi.
Kukatazwa Kilimo cha kujikimu (Bustani) ili hali ukame wa 2008/2009 ukiwa umepukutisha Mifugo mingi ya Wafugaji kunawafanya Wamaasai hao hivi sasa kulia njaa huku wengine mlo wao ukiwa ni Mahindi ya kuchemsha, majani pori na maziwa.
Kuna kundi kubwa linaishi kwa kutegemea msaada wa Chakula. Na wanachodai hivi sasa ni kurejeshwa kwa kilimo cha kujikimu wakiamini kuwa hawawezi kuharibu mazingira kama ambavyo Serikali inahofia.
KUMRADHI/MAREKEBISHO:
Mzungumzaji wa Mwisho ni Mheshimiwa Balozi Khamis Kagasheki ambaye ni Waziri wa Maliasili na Utalii
Негізгі бет NILICHOKISHUHUDIA NGORONGORO KUHUSIANA NA NJAA
Пікірлер: 9