Polisi eneo la Embu mashariki wanawazuilia wanafunzi 28 ambao walipatikana ndani ya baa tofauti mjini Runyenjes jana usiku. Kulingana na naibu kamishna wa eneo hilo Jane Waruinge, wanafunzi hao wataendelea kuzuiliwa wakisubiri wazazi wao ili kupewa ushauri nasaha. Aidha ameonya kwamba baa zote eneo hilo zitafungwa iwapo hazitafuata masharti ya kutowaruhusu watoto walio chini ya miaka 18. Aidha wazazi wameonywa dhidi ya kutotekeleza wajibu wao wa kutoa malezi bora.
- Күн бұрын
Polisi eneo la Embu mashariki wawazuilia wanafunzi 28 ambao walipatikana ndani ya baa tofauti
- Рет қаралды 1,365
Пікірлер: 1