Dar es Salaam. Mtaalamu na mbobezi wa masuala ya sheria, Profesa Abdallah Safari amefichua siri ya kujiweka kando na shughuli za kisiasa badala yake ameamua kukitumia ipasavyo kipawa chake cha utunzi wa vitabu.
Profesa Safari aliyewahi kuwa kada na mshauri wa masuala muhimu ya kisheria wa Chama cha Wananchi (CUF), anasema akijitosa katika siasa hivi sasa atajitoa kafala, ndio maana amejiondoa huko akidai hakuna watu makini.
Mwanazuoni huyo ameeleza hayo wakati wa mahojiano wa maalum na Mwananchi Digital lililotaka kujua masuala mbalimbali yanayomhusu katika nyanja za siasa, taaluma ya sheria na uandishi wa vitabu.
Негізгі бет Profesa Safari aelezea sababu ya kujitenga na siasa, asema "Siwezi kuwa chawa, najitoa kafala"
Пікірлер: 86