Tofauti na malumbano kati ya waziri mkuu na wabunge waasi wanaoongozwa na mbunge wa eldoret kaskazini william ruto, yalijitokeza tena wazi bungeni alasiri hii. Majibizano ya maneno, yaliibuka, wakati wa muda anaotengewa waziri mkuu bungeni kila jumatano, kusutana kuhusiana na tofauti kuanzia masuala ya icc, katiba na kubadilika kwa misimamo kuhusiana na kuundwa kwa mahakama maalum hapa nchini. Waaasi hao walimkosoa waziri mkuu kwa kuwakejeli kuwa hawana haki ya kuzungumzia katiba ilhali walikuwa mstari wa mbele kuipinga wakati wa kura ya maoni. Waziri mkuu naye alijitetea akisema waasi hao wamekuwa wakieneza propaganda kuwa yeye anahusika na masaibu ya washukiwa kupelekwa huko the Hague.
Негізгі бет Raila vs Ruto Parliament battle
Пікірлер: 24