Rais waJamhuri ya Zambia Mhe. Edgar Chagwa Lungu leo tarehe 27 Novemba, 2016 majira ya jioni amewasili hapa nchini kwa ziara ya kiserikali ya siku 3 kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Rais Lungu amepokelewa na mwenyeji wake Rais Magufuli na kulakiwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa RaiswaJamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali hapa nchini pamoja na wananchi.
Негізгі бет RAIS DKT MAGUFULI AMPOKEA RAIS WA ZAMBIA MHE EDGAR LUNGU, NOV 27,2016
No video
Пікірлер: 1