Rais John Magufuli amevunja ukimya juu ya sakata la shilingi trilioni 1.5 akisema anashangazwa na taarifa kuwa fedha hizo hazijulikani zilipo.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kuwaapisha majaji wapya, Naibu Mwendesha Mashtaka, Wakili Mkuu na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali aliowateua hivi karibuni.
Katika hotuba yake, Rais Magufuli pia ameonya juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii akisema “Kuna ugonjwa umeingia kwa sasa Watanzania kuamini kila kinachoandikwa kwenye mitandao ni kweli.
Kwa bahati mbaya Tanzania hatuna uwezo wa 'Control' hili mitandao. Ndiyo maana taarifa zinasambaa wakisema, mishahara ya majaji imeshuka, fedha za maendeleo zimeshuka.
"Pia kuna taarifa ya kupotea kwa shilingi Trilioni 1.5, lakini katika taarifa niliyopokea sikuambiwa na CAG kuwa kuna fedha zimepotea..., huu upotoshaji unaweza kutusababisha madhara makubwa."
Негізгі бет Rais Magufuli awajibu wanaodai kupotea kwa Tsh. trilion 1.5, atoa onyo
Пікірлер: 74