Rais mstaafu Uhuru Kenyatta ametoa maelezo zaidi kuhusu idadi ya bunduki zilizoko mikononi mwa familia yake. Uhuru akisema wanawe wa kiume wana bunduki tatu kila mmoja tofauti na taarifa ya serikali kwamba familia hiyo ina bunduki 23. Pia Uhuru ameonekana kutumia fursa hii kufafanua zaidi kuhusu yaliyosibu familia yake siku za punde. Alitoa maelezo hayo katika kikao na wahariri akiwa afisini mwake hapa jijini Nairobi.
Негізгі бет Rais mstaafu Uhuru Kenyatta asema wanawe wana bunduki 6
Пікірлер: 386