Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Burian amelitaka jeshi la polisi mkoani humo kufanya kazi Kwa kuzingatia haki na weledi na kuwaasa waache vitendo vya rushwa ambavyo vitaweza kulichafua jeshi hilo nchini.
Balozi Dkt Batilda ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya usalama mkoani Tanga, ameyasema hayo kwenye hafla ya kuwatunuku vyeti na Tuzo askari Saba wa jeshi hilo kwa niaba ya wengine ambao wamefanya vizuri katika majukumu yao ya utendaji
"Fanyeni kazi zenu kwa haki, weledi mkizingatia tunu za Viongozi wetu Ili matukio tunayoyaona Kwa wenzetu yasiweze kutokea nchini kwetu," amesema Dkt Batilda
Dkt Batilda amesema askari wakitekeleza majukumu yao kwa haki na weledi huku wakitumia mbinu bunifu za kisayansi kupambana na uhalifu kutaongeza sifa kwa jeshi hilo.
Akizungumza mara baada ya Hafla hiyo Kaimu Kamanda wa polisi mkoani Tanga, ACP Maket Msangi amesema jumla ya askari Saba mkoani hapa wamepewa tunzo na sifa kutokana na utendaji wao wa kazi miongoni mwa askari waliopo mkoani hapa kutokana na kuchunguza na kuzuia uhalifu katika maeneo yao ya kazi.
Amesema watatekeleza yale waliyoagizwa na Mkuu wa mkoa lakini pia wataendelea kupambana na uhalifu huku wakizingatia maelekezo hayo ya Mkuu wa mkoa.
Негізгі бет RC TANGA ASISITIZA WELEDI WA KAZI KWA JESHI POLISI
Пікірлер