#SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
ASKARI WA BRIGEDIA
Mbele ya macho ya wengi Nape Mosses Nnauye ni kama SIMBA, anatisha, amejaa, anajiweza na anajitambua na kutambua kile akifanyacho na yake yote anayoyasema na kuyafuatilia. Na kwenye macho ya wale wa karibu yake Nape ni yote hayo na zaidi ni mtu mwenye mapenzi ya dhati kwa wale wa karibu na moyo wake, mcheshi, anapenda watu na ni rafiki wa kweli, yule rafiki mmoja ambaye haijalishi kukoje ila yeye ndiye ambaye atabaki na wewe mpaka mwisho, na atakuambia ukweli pale panapohitajika.
Mimi na yeye ni mtu na mdogo wale ambao wamepishana kama miaka minne hivi, huwa tunawasiliana na kuongea tunapokutana, tunaheshimiana na kuaminiana pia. Ila kwa respect ili tuweze kumpata kwenye mazungumzo haya tuliamua kumtumia mdogo wake Kipenzi anayeenda kwa jina la Bimdo ili hata kama alikua na mambo mengi kiasi gani, au ratiba yake imebana ki vipi, basi kwa wawili sisi angefanya linalowezekana ilimradi atufurahishe, na tulifanikiwa 😄.
Baba na mume na Kaka na Kiongozi kwa watu wake wa Mtama, Nape ni moja ya nguzo imara za Chama Cha Mapinduzi, naamini mpaka leo bado iko hivyo, kipindi cha uchaguzi wa Mwaka 2015 ndo tulimuona zaidi, wakati Chama chake pendwa kilipokua kinakabiliwa na upinzani wa mkubwa kutoka kwa vyama vyengine vya Siasa. Nape yeye ndo alikua mstari wa mbele wa kupanga mashambulizi na mipango sahihi ya kuweza kupata mgombea sahihi ambaye Chama kingemsimamisha na kuweza kupata dhamana kutoka kwa wa Tanzania zaidi ya milioni 55 ambao kwa hamu tulikua tukingojea kutambua jina na mtu ambaye Chama kingempa dhamana. Haikua mechi ndogo Ila kama tunavyofahamu sasa imebaki story tu. CCM walimsimamisha Hayati Dr John Pombe Joseph Magufuli na mambo mengine mengi yakaanzia hapo.
Sasa hayo mambo mengine mengi yaloanzia hapo ndo moja ya sababu nyingi zilizotufanya sisi tutake kuongea na Nape, akiwa imara na alojaa tabasamu yeye hakua na hiyana kujibu maswali yetu mengi ya kutaka kujua mawazo yake juu ya mambo mengi ambayo kama Taifa na yeye kama mwanasiasa tulipitia. Kuanzia jinsi CCM ilivyoshinda uchaguzi, teuzi, kutumbuliwa, issue ya aliyekua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kipindi hicho, mambo ya kutolewa silaha hadharani, issue ya yeye kwenda Ikulu kuomba msamaha, miaka 6 ya JPM na Tanzania kama taifa na mueleko wake, niamini nikisema humu yote tuligusia na yeye alitujibu.
Nape ni mmoja ya watoto wa Marehemu Brigedia Mosses Nnauye, mmoja wa watu imara sana wa nchi hii, pia tulitaka atuambie mahusiano yake na Marehemu Mzee wake, kama kuna lolote amejifunza kutoka kwake na kama yeye ndo alikua chachu ya yeye kuwa anafanya ayafanyayo sasa (kutumikia wananchi wake wa Mtama) na alituelezea kwa kirefu tu juu ya wasifu wa Mzee wake.
Kuna mahusiano yake pia na Marehemu Ruge Mutahaba, ukaribu wake na January Makamba na Zitto Kabwe, events za miaka minne mitano iliyopita zimemfunza nini hasa? Majibu yote ya maswali tele tulokua nayo, Nape alitupatia. Yangu matumaini nawe uta enjoy mazungumzo haya kama sisi tulivyo enjoy.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
KZitem Link bit.ly/KZitemS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: instagram.com/slidedigitaltz
Негізгі бет Salama Na NAPE NNAUYE SE6 EP15 |ASKARI WA BRIGEDIA PART 1|SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Пікірлер: 32