Kilichoanza kama amri ya mahakama kwa maafisa wa upelelezi kubaini iwapo kuna watoto waliofariki au kuuawa katika shughuli za kanisa la Good News International kiligeuka kuwa uchunguzi wa mauaji mabaya zaidi yaliyowahi kufanyika nchini Kenya katika siku za punde. Zaidi ya maiti 240 za wafuasi wa mhubiri tata Paul Mackenzie zimepatikana katika msitu wa Shakahola kaunti ya Kilifi hadi kufikia sasa. Mwanahabari wetu Hassan Mugambi alikuwa Shakahola na ametuandalia makala maalum kuhusu ni vipi waumini hawa walifika msitu huo, na hata namna walivyoishia kuaga dunia.
Негізгі бет | SIRI YA SHAKAHOLA | Picha ya ndani ya msitu wa Shakahola
Пікірлер: 322