Jinsi ya kutumia ATM
Unapo fungua akaunti ya benki, benki yako itakupa kadi kama hii.
Inaitwa kadi ya benki. Benki tofauti zina kadi za rangi tofauti.
Unapo itisha kadi ya malipo, itabidi uchague nambari.
Hii inaitwa PIN yako. Ni muhimu kukumbuka nambari yako kwani utahitaji kuitumia wakati wowote unapo tumia kadi yako. Usishiriki nambari hii na mtu yeyote.
Unapo kwenda dukani, unaweza kutumia kadi hii kununua vitu, kisha pesa huondolewa kwenye akaunti yako ya benki.
Unaweza pia kwenda kwenye mashini, inayoitwa ATM ili kupata pesa kutoka kwa akaunti yako ya benki. Pia, ATM inaweza kuku-onyesha pesa ngapi zinasalia kwenye akaunti yako ya benki.
Kwa kawaida unaweza kupata ATM kwenye kituo cha mafuta ya gari, na pia benki. Unaweza kutozwa ada ikiwa hutumii ATM ya benki yako mwenyewe.
Video hii itakuonyesha jinsi ya kutumia ATM.
Unapofika kwenye ATM angalia mazingira yako ili kuhakikisha kuwa uko salama.
Hakikisha uko katika eneo lenye mwanga. Ikiwezekana, tumia ATM wakati wa mchana.
Kuna sehemu ya kadi yako ya malipo inayoitwa "CHIP",
Hivi ndivyo inavyoonekana.
Ingiza kadi yako kwenye ATM huku chipu ikitazama mbele.
Ikiwa umeingiza kadi kwa njia sahihi, hutaweza kurudishiwa kadi, hadi umalize kupokea pesa zako.
Ukiweka kadi kwa njia isiyo sahihi, kadi itasukumwa nje,kwa hivyo igeuze tu, na ujaribu tena.
ATM inaweza kukuuliza uchague lugha unayozungumza. Kuna chaguo chache tu za lugha na kuna uwezekano mkubwa yakuwa lugha yako haitakuwa mojawapo.
Katika video hii tutachagua Kiingereza, kama hii.
ATM itakuuliza uweke nambari yako ya siri. Unapoingiza nambari yako ya PIN, hakikisha kuwa umeficha pedi kwa mkono wako ili watu wengine walio karibu wasiweze kuona unachofanya.
Ukishaweka nambari yako ya siri, ATM itakuuliza unacho hitaji kufanya.
Unaweza kuchagua:
pesa za haraka, kutoa pesa, au kuangalia salio la akaunti.
Pesa kutoka kwa ATM kawaida huja kwa bili $10 au $20.
Ikiwa unaomba kiasi kikubwa cha pesa, unaweza kupata bili ya $ 100.
Unapobonyeza Kutoa pesa, itakuruhusu kupokea kiasi halisi cha pesa.
Kwa mfano.
$30, $70, $150.
Kwa kawaida kuna kikomo cha kiasi cha pesa unachoweza kuchukua kwa wakati mmoja kwa siku moja. Hutaweza kamwe kuchukua pesa zaidi ya zile ulizo nazo kwenye akaunti yako ya benki.
Kuna vile ATM ikuulize ikiwa unataka risiti iliyochapishwa.
Hii inakuonyesha ni pesa ngapi umetoa na, ni pesa ngapi umebakisha kwenye akaunti yako.
Chagua "Ndiyo" ili kupata nakala iliyochapishwa, au,
Chagua "Hapana" ikiwa hutaki risiti iliyochapishwa.
Iwapo ungependa kujua ni kiasi gani cha pesa kilicho kwenye akaunti yako ya benki, unaweza kuchagua vitufe vya "Maswali ya Mizani" kwenye upande wa skrini.
"Salio" linamaanisha kiasi cha pesa kwenye akaunti yako ya benki hivi sasa.
Salio lako litaonyeshwa kwenye skrini.
Baadhi ya ATM zita simamisha biashara yako, mara tu utakapopokea pesa zako.
ATM zingine zinaweza kukuhitaji ubonyeze alama X ilio nyekundu kwenye pedi ya pini,
au ubofye kitufe kinachosema mwisho.
Kuna ATM nyingi ambazo hazitakupa pesa zako hadi kadi yako iondolewe kwenye mashine.
Ni rahisi kusahau kuchukua pesa,
kadi au risiti yako ukiwa na haraka.
Hakikisha umekamata zote hizi, na uziweke salama kabla ya kuondoka kwenye ATM
Ukisahau kadi yako, rudi kwenye ATM mara moja ili uichukue.
Ikiwa kadi yako haipo, au imepotea au kuibiwa, mara moja, nenda kwa benki yako au uwapigie simu na uwajulishe.
Benki itasimamisha kadi yako kutumiwa na mtu mwingine yeyote mara hiyo hiyo, na kukupa kadi mpya ya malipo.
Негізгі бет SWAHILI: Jinsi ya kutumia ATM How to Use an ATM
Пікірлер