Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutekeleza mradi wa Ujenzi wa daraja la JPM (Kigongo-Busisi) lenye urefu wa KM 3.2 linalojengwa na mkandarasi China Civil Engineering Construction Corporation (CCECC) kwa gharama ya zaidi ya Tshs. Bilioni 716.
Hayo ameyasema leo juni 10, 2024 alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa daraja la kigongo - Busisi ambapo amesema chini ya usimamizi wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Mwanza, ujenzi wa daraja hilo umefikia asilimia 88.2 na akatumia wasaa huo kuwapongeza kwa kazi nzuri.
"Nimeona kazi nzuri mnayoifanya, ninawapongeza sana na ninatoa wito kuendelea kusimamia vizuri na kwa kasi ile ile ili mradi huu ukamilike kwa wakati ifikapo disemba 30 mwaka huu".
Mtanda ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kujenga daraja hilo kwa kasi kwani Rais Samia amelikuta likiwa chini ya asilimia 40 kiujenzi na hata malipo ya fedha lakini ndani ya miaka mitatu limeendelezwa bila kusimama na kwamba sasa wananchi wataondolewa adha ya msongamano kwenye vivuko.
Ameongeza kuwa kukamilika kwa daraja hilo kutatoa fursa kwa mikoa ya Kanda ya ziwa na nchi za jirani kuwa na hakika wa kufika kwa urahisi vilevile utasaidia kupunguza msongamano w magari kwenye vivuko vinavyotumika sasa na kwamba utarahisisha suala la usafiri kwa ujumla.
Mwakilishi wa Meneja wa TANROAD Mkoa huo Mhandisi Richard Ruyango amesema awali ujenzi wa daraja hilo linalogharimu ulioanza mwaka 2020 ulitarajiwa kukamilika mwezi februari mwaka huu lakini kutokana na sababu mbalimbali mkandarasi huyo aliongezewa muda.
"Hatujaona mpango wa kujenga mzani upande wa Sengerema hivyo tunaomba ujengwe ili kulinda daraja letu maana uwekezaju huu ni lazima ulindwe kwa kuweka ukomo wa uzito wa magari kupita ili lidumu muda mrefu." Mhe. Hamis Tabasam, Mbunge wa Sengerema.
Негізгі бет TAARIFA NYINGINE KUBWA HII HAPA IMETUFIKIA LEO KUTOKA MWANZA KUHUSU DARAJA LA MAGUFULI
Пікірлер: 21