" Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina Upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu... Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni Upendo"
"Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo"
"Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake"
Wapendwa, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.
Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo.
(Korintho, 13:1.., 1 Yohana 3:1, Yohana 15:13, 1 Yohana 4:7..)
Негізгі бет "Tazameni, ni Pendo la namna gani alilotupa Baba.."
Пікірлер