Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imelaani kitendo cha video inayosambaa katika mitandao ya kijamii inayoonyesha vijana watano wakimbaka na kumlawiti binti na ambapo imesema kitendo hicho sio cha kiungwana na hakikubariki popote.
Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora JajiMstaafu Mathew Mwaimu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye banda la tume hiyo lililopo katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzunguni.
Негізгі бет THBUB YATOA TAMKO ZITO JUU YA VIDEO YA UKATILI INAYOSAMBAA MITANDAONI
Пікірлер