Timu 10 zimethibitisha rasmi kushiriki ligi ya Ngende cup 2024 itaanza kutimua vumbi Juni 12,2024 katika wilaya ya Liwale mkoani Lindi.
Siraji Kimbinda ni katibu wa chama Cha mpira wilaya ya Liwale (LIDIFA) amezitaja timu zilizothibisha kushiriki ligi ya Ngende cup ni timu ya Liwale B. fc, Likongowele fc,Liwale united,Kona Mbaya fc,Home Boys fc.
Timu zingine ni Mangirikiti fc, Mungurumo fc,Mifugo fc,Kasino fc na Mamelod Sundown.
Mdhamini wa ligi ya Ngende cup 2024, Shomari Ngunduli ambapo kwenye mashindano hayo amebanisha zawadi kwa mshindi wa kwanza atajinyakulia fedha taslimu milioni Moja (1,000,000),mshindi wa pili atapata shilingi laki tano (500,000) na timu zitakazotinga nusu fainali jezi seti Moja na mpira.
Zawadi zingine ni kwa golikipa bora atapata gloves pea moja,kocha bora atapata shilingi laki Moja (100,000),mfungaji bora atapata viatu pea moja na mchezaji bora atapata mpira mmoja.
Kwa upande wake msimamizi wa ligi Juma Kamkosa amesema zawadi zote pamoja na maandalizi ya mpira yamekamilika kwa asilimia 100.
Viongozi wa timu wamejadiliana kanuni za uendeshaji wa ligi ya Ngende cup 2024 tayari kwa kuanza ligi rasmi juma tano ya Juni 12 2024 kwa upande wake Karimu Libena na Wabaki Bakiri wamesema ligi imekuja muda mwafaka kwa wachezaji kuonesha vipaji vyao huku wakifurahia zawadi zitakazotolewa kwenye ligi hiyo.
kundi A
1.Liwale united fc
2.Liwale B fc
Likongowele fc
4.mamelod sundown
5.mangirikiti fc
kundi B
1.Kasino fc
mungurumo fc
3.Kona Mbaya fc
4.Mifugo fc
5.Home boys fc
Негізгі бет TIMU 10 ZIMETHIBITISHA KUSHIRIKI LIGI YA NGENDE CUP 2024-LIWALE
Пікірлер