NYIMBO ZA WOKOVU #140
Verse 1
Ukichukuliwa na mashaka yako
Na kuona hufu kwamba utakwama,
Uhesabu mibaraka yake Mungu,
Na utashangaa kwa rehema yake
Chorus
Uhesabu mibaraka yote
Mungu aliyoyakubariki!
Ukumbuke mambo yote pia,
Na utashangaa kwa rehema yake!
Verse 2
Na ukiudhiwa na huzuni nyingi,
Ukiona msalaba ni mzito,
Uhesabu mibaraka kuchwa pia,
Na kwa moyo wote utasifu Mungu
Chorus
Uhesabu mibaraka yote
Mungu aliyoyakubariki!
Ukumbuke mambo yote pia,
Na utashangaa kwa rehema yake!
Verse 3
Wengi watamani mali ya dunia;
Utajiri wako ni Mwenyezi Mungu.
Uhesabu mibaraka na kumbuka:
Mali haiwezi kufungua mbingu
Verse 4
Na katika mambo yote huku chini
Ukumbuke pendo kubwa la Mwokozi!
Na ujumlishe mibaraka yote,
Tena mwisho atakuchukua kwake!
Chorus
Uhesabu mibaraka yote
Mungu aliyoyakubariki!
Ukumbuke mambo yote pia,
Na utashangaa kwa rehema yake!
Негізгі бет UFUNUO WAKO #1: Uhesabu mibaraka yote _ Emmy Niyonzima
Пікірлер: 64