Watu watatu waliojitambulisha kuwa wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamekamatwa leo Jumatatu Septemba 23, 2024 wakifanya mahojiano na waandishi wa habari eneo la Ilala Boma, jijini Dar es salaam.
Septemba 11, 2024 Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kufanyika maandamano ya kulaani matukio ya watu kutekwa na kuuawa, akiwemo aliyekuwa kada wake, Ali Kibao. Hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, David Misime lilitangaza kuyapiga marufuku.
Kwa mujibu wa Mbowe, wameamua kuweka mkazo wa suala hilo, baada ya maombi ya mahitaji, ikiwemo kutaka kujiuzulu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni, viongozi waandamizi wa ulinzi na usalama kama sehemu ya uwajibikaji.
Негізгі бет WAFUASI WA CHADEMA WATEMA NYONGO, WADAKWA
Пікірлер: 22