Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Balozi Dkt. Batilda Burian amekabidhi magari manne yakiwemo magari matatu kwa Wakuu wa Wilaya ya Kilindi , Pangani na Korogwe na gari moja kwa ajili ya usimamizi wa ofisi ya mkuu wa mkoa yakiwa na thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 833.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi magari hayo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe Balozi Dkt. Batilda Burian amewataka Wakuu wa Wilaya waliopata magari hayo kuyatumia katika kuwafikia Wananchi na kutatua Kero zao sambamba na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo.
Imeandaliwa na Emma Kigombe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga
Негізгі бет WAKUU WA WILAYA TANGA WAKABIDHIWA MAGARI MAPYA
Пікірлер: 3