Wamiliki wa magari ya shule wilaya ya Misungwi wamelipondeza Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza kwa kuendelea na zoezi la ukaguzi wa magari linaloendela Jijini humo.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo linalofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Nyang'omango wilayani Misungwi kwa niaba ya wamiliki wa shule binafsi mkuu wa shule ya Rishor iliyopo Usagara, mwalimu Jackson Baraza amepongeza Jeshi la Polisi kwa namna linavyoenesha zoezi hili.
"Usalama wa haya magari ni jambo la msingi sana, tunalishukuru Jeshi la Polisi kwa kuendelea kukagua mifumo ya magari yetu na tunaomba zoezi hili lisihishie hapa liwe endelevu" amesema Baraza
Naye, Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani wilaya ya Misungwi (DTO) Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Michael Mwakasungura amesema wanaendelea kutekeleza maelekezo ya ukaguzi kama walivyoelekezwa na kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza.
Ukaguzi huu ni kutekeleza maelekezo ya kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Afande Wilbrod Mutafungwa (DCP) wakati anafungua zoezi hili kimkoa alitutaka ma DTO's kuhakikisha tunasimamia zoezi hili la ukaguzi wa magari kikamilifu" amesema Mwakasungura
Kwa upande wake Mkuu wa Polisi wilaya ya Misungwi Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Oscar mmole amewahimiza wakaguzi wa magari kuhakikisha wanakagua vizuri mifumo yote na magari yatakayobainika ni mabovu wahakikishe yanatengezwa kabla ya kuingia barabarani.
"Niwaombe wamiliki wa magari binafsi hili zoezi liwe endelevu tusiwe tunalitekeleza kwa maelekezo tu wewe mwenyewe binafsi ukiona gari lako ni bovu basi lilete kituo cha Polisi ili liweze kufanyiwa ukaguzi" amesema SSP Mmole
Akiongea kwa niaba ya madereva waliofika eneo hilo kwaajili ya ukaguzi wa magari yao Mussa James amesema wamelipokea zoezi hilo na limekuwa darasa kwao kwani linaenda kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.
Zoezi hilo lilizinduliwa Juni 24, 2024 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) Wilbroad Mutafungwa ambapo aliwaelekeza wakuu wa Polisi wilaya kupitia mkuu wa kikosi cha usalama barabarani kufanya ukaguzi wa magari huo huku wakizingatia mambo kadha ikiwemo uchakavu wa ‘bodi’ la gari, matairi, uwepo wa mikanda kwenye viti vya abiria, taa, leseni ya dereva iliyo hai, umahiri na ufanisi wa dereva ikiwemo ‘uoni wa dereva’ na uwepo wa mwangalizi wa wanafunzi ‘Matroni/Patroni' katika gari husika.
Kutoka Dawati la Habari Polisi Mwanza
Негізгі бет WAMILIKI WA SHULE BINAFSI WAPONGEZA POLISI KWA UKAGUZI WA MAGARI YA SHULE WILAYA YA MISUNGWI.
Пікірлер