Kuelekea mchezo wa kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika kati ya Tanzania na Lesotho Novemba 18 mwaka huu, kipindi cha Wednesday Night Live leo kimewaalika magwiji wawili wa soka la Tanzania waliokuwa sehemu ya timu iliyofuzu michuano hiyo mwaka 1980.
Hawa si wengine, ni golikipa Juma Pondamali na Peter Tino ambaye ndiye aliyefunga bao lililoifanya Tanzania ifuzu michuano hiyo.
Magwiji hawa wamezungumza mengi ikiwemo kueleza kilichofanyika wakati huo hadi Tanzania ikafuzu, lakini pia wametoa ushauri nini kifanyika ili kuboresha soka la Tanzania.
Kipindi hiki ni kila Jumatano saa 3:30 usiku Azam Sports 2 chini Patrick Nyembera.
Негізгі бет WEDNESDAY NIGHT LIVE 14/11/2018: Peter Tino, Pondamali wafichua kilichoipeleka Tanzania AFCON 1980
Пікірлер: 6