Makundi Nyimbo: Kwaresma na Toba (Lent & Repentance)
MANENO YA WIMBO
1. Yesu kanikuta jangwani, akaniambia, nenda huko Yerusaleme
Yesu kanikuta gizani, akasema, kimbilia Yerusaleme
Mimi ni kipofu ni mauti (mimi ni mauti)
Mimi ni kipofu sioni (mimi sioni)
{ Kulikuwa giza, kukapambazuka
Nikamwona Bwana Bwana wangu }*2
2. Natamani mji ule, Yerusaleme kuna nuru kuna raha
Dhambi zangu matendo yangu, ni maovu, tazameni msalabani
Upindo wa nguo (nguo yako safi)
Upindo wa nguo (nguo yako nzuri)
{ Uniguse moyo, moyoni mwangu
Nitaimba sifa sifa zako } *2
3. Watakatifu wa moyo, tumsifuni, Bwana mwenye nchi na mbingu
Twende huko nchi ya mbali, ya Kanaani ndiko tutaishi milele
{ Fimbo yake Musa ilituokoa
Fimbo yake Musa, ilituongoza
{ Nchi ile ya Misri (nchi ya farao)
Tulimwona Bwana mwenye enzi } }*2
#wanaromano
#kwaresma
Негізгі бет YESU KANIKUTA JANGWANI (Lent & Repentance) || Kwaya Mt. Romano Mtunzi
Пікірлер: 30