CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Iringa Mjini kimemtangaza Mch Peter Msigwa kuwa hasimu na adui wa demokrasia nchini kikiwataka wanachama na wafuasi wao kumuogopa kama ukoma.
Akitoa msimamo wa chama hicho unaopuuza wito unaowataka baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho kujiunga naye CCM, Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Iringa Mjini, Frank Nyalusi alisema watahakikisha wanapambana naye usiku na mchana ili kuilinda demokrasia na kutetea haki za watanzania.
Akizungumza na wanahabari ndani ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya Jimbo la Iringa Mjini kilichohudhuriwa na viongozi wa kata zote za jimbo hilo leo, Nyalusi alisema; "Kuondokewa na Mchungaji Msigwa, kumekifanya chama chetu kuwa salama kuliko ilivyokuwa jana. Hii ni kama meli, wanashuka abiria wawili wanapanda wapya 200."
Alisema wanachama na viongozi wa jimbo hilo wanaingia rasmi kazini ili kujihakikishia zaidi ushindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani ambao wana imani utabebwa na nguvu ya umma.
"Chadema hatutaki kumfanya Mch Msigwa kuwa ajenda yetu, hatutamzungumzia lakini tutajibu hoja zake dhidi yetu na kwa kinachoendelea huko mitandaoni nadhani amekwishaanza kuonja joto la jiwe," alisema.
Alisema Chadema ni tanuli la kutengeneza viongozi na kama Mch Msigwa alivyopikwa na akaiva akiwa ndani ya chama hicho, kinao wanachama na wafuasi wengi wanaoweza kufanya kazi zaidi ya ile iliyofanywa na Mchungaji huyo wakati akijitambua katika kutetea maslai mapana ya Taifa hili.
"Niwatoe hofu wapenzi na wafuasi wa mabadiliko, tunakwenda kushinda kwa kishindo uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani kwasababu tunahakika Msigwa na chama chake bado hawawezi kuzipatia majibu hoja nyingi za wananchi," alisema.
Aidha chama hicho kimezungumzia kampeni chafu inayodaiwa kufanywa na baadhi ya wanachama wake wanaowarubuni baadhi ya wanachama wao ili wajiunge na CCM kwa kisingizio cha kumfuata Mch Msigwa kikisema kinafuatilia na kitachukua hatua.
Негізгі бет CHADEMA IRINGA WAMTOLEA UVIVU MSIGWA, "HUYU NI ADUI YETU KUANZIA SASA"
Пікірлер: 5