Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, *Mhe Albert Chalamila*Agosti 17,2023 amevunja uongozi wa Soko la Mabibo na kuagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU} kufanya uchunguzi wa kina katika soko hilo na watakao bainika hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
RC Chalamila ametoa alipofika katika soko hilo kutatua mgogoro baina ya wafanyabishara biashara wasiowaaminifu wakiongozwa na Uongozi wa Soko hilo na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
Aidha RC Chalamila amekemea watu wachache, wabinafsi, katika soko hilo kukwamisha jitihada za serikali na kamwe wasijaribu hata kidogo masoko lazima yaboreshwe Serikali ikusanye mapato yake na wafanyabishara wafanye biashara zao sehemu rafiki.
"Hatuwezi kuacha watu wachache wanajinufaishe na Serikali inakosa mapato, Mkurugenzi wa Manispaa anza kazi leo," Alisema Chalamila
Негізгі бет CHALAMILA ACHEFUKWA SOKO LA MAHAKAMA YA NDIZI
Пікірлер: 6