#dullysantz #santzmedia #maulidkitenge#kitengetv #maulidkitenge #mfahamumaulidkitenge
Maulid Baraka wa Kitenge ni mtangazaji wa Efm redio
Sifa yake kuu inatokana na machachari aliyonayo hasa maswali yake ya kukwaza, wakati akiongea na vyanzo vya habari mbalimbali ili kusaka ukweli wa jambo fulani.
Maulid Baraka wa Kitenge ni mtangazaji anayetajwa kuwamo kati ya walio bora, wanaotangaza vipindi vya michezo kwenye redio na televisheni nchini.
Sifa yake kuu inatokana na machachari aliyonayo hasa maswali yake ya kukwaza, wakati akiongea na vyanzo vya habari mbalimbali ili kusaka ukweli wa jambo fulani.
Ikiwa ametimiza miaka 15 katika fani ya utangazaji, Kitenge amewahi pia kuyaandikia magazeti ya Alasiri na Lete Raha, Kitenge amewahi kutangaza vipindi vya Nipashe na Kumepambazuka kwenye Kituo cha Radio One, ambavyo si vya michezo.
Tofauti na kipindi cha Spoti Leo ambacho kinatajwa kusababisha Kitenge kuwa nyota kwenye eneo hilo la utangazaji.
Kwa sasa Kitenge ni mmoja wa watangazaji wanaokiwakilisha kituo kipya cha masafa mafupi (FM) cha Radio Efm, akiwa mtangazaji wa kipindi cha michezo kinachorushwa hewani kwa saa tatu, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia kuwa na kipindi cha michezo cha muda mrefu kuliko vyote nchini kinachorushwa hewani asubuhi.
Mtangazaji huyo, bado anatajwa kuwa mdau mkubwa wa michezo nchini na gazeti hili lilifanya mahojiano naye na anaeleza safari yake ya utangazaji wa michezo.
Ndoto ya utangazaji, kuiga sauti ya Liongo
Akieleza alivyoguswa na kuvutika katika utangazaji Kitenge anasema: "Ilikuja baada ya kuandika zaidi habari za michezo, nikawa napeleka taarifa kwenye kipindi cha michezo cha Redio One, wakati huo mtangazaji alikuwa Aboubakar Liongo. Nilipenda utangazaji wake, baadaye nikachukuliwa niingine kwenye fani na kuanzia hapo nikatengeneza jina langu redioni."
Anasema kwa kumtumia Liongo alitengeneza njia yake, kwani alimfanya kuwa rafiki na kujifunza kwake hasa masuala ya utendaji.
Mtangazaji huyo aliwahi kukumbwa na tuhuma kutoka mashabiki wa michezo kwamba anatangaza akimuiga zaidi Liongo.
Hata hivyo, Kitenge anakiri kutokea kwa hali hiyo akieleza: "Ni kwa sababu nilikuwa namtumia Liongo kama njia yangu ya kufika kwenye mafanikio. Hivyo kuna vitu nilichukua nami nikaongeza vyangu na maisha yakaendelea."
Anaongeza: "Nakiri kuna kipindi nilikuwa napita kwenye reli zake, nikawa namuiga, lakini baada ya kufanikiwa nami sasa nina aina yangu ya utangazaji. Nililofanya halikuwa kwa nia mbaya, bali kwa nia njema na nimefanikiwa kufika nilipo sasa. Kumbuka, alipoondoka yeye (Liongo), mimi nikawa ndiyo mtangazaji mkubwa hasa wa michezo na leo Maulid Kitenge anajulikana kama Maulid Kitenge na siyo Maulid anayemuiga Liongo."
Wakati mgumu
Alipotakiwa kueleza wakati upi ulikuwa mgumu kwenye maisha yake ya kazi Kitenge anaeleza kwamba katika miaka 15 alipokuwa Radio One, alifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na wafanyakazi wenzake, akiishi kwa amani hadi alipoondoka na kuhamia kituo cha Efm.
Hata hivyo anasema kwamba anakumbuka siku moja alipopatwa na wakati mgumu ambao hataweza kusahau.
Ni hivi... Siku hiyo alipata habari kwamba Mwenyekiti wa IPP, ambaye ndiye mmiliki wa Radio One, amepata habari kwamba yeye (Maulid) ni rafiki mkubwa wa Yusuph Manji, aliyekuwa hasimu wa Mengi.
"Nilikosa raha kabisa, tena wakati huo Manji nilikuwa sijawahi kuonana na Manji. Habari hizo zilifanya niione ofisi ya moto, mbaya zaidi nilipata hizo habari kutoka kwa mkurugenzi wetu, Joyce Mhaville," anasimulia Kitenge.
Uamuzi Mgumu
Mbali ya tukio hilo, Kitenge anabainisha kuwa maishani mwake hakuwaji kufanya uamuzi mgumu kama kuhama kutoka Redio One na ITV kwenda Efm kituo ambacho ndiyo kwanza kilikuwa kimeanzishwa.
"Haikuwa kazi rahisi kuhama kutoka katika kituo unachoamini kuwa ndicho kilichokulea. Siku nilipopigiwa simu na mtangazaji mwenzangu, Ssebo kuhusu kujiunga na Efm, nilijua kuna kitu tofauti kinataka kutokea katika maisha yangu," alisema Kitenge na kufafanua:
"Ni kama mtoto kumwacha mzazi aliyemlea. Haikuwa kazi rahisi, lakini ilinibidi kuamua. Mmoja kati ya watu niliowafuata kuomba ushauri alikuwa ni Charles Hillary. Yeye aliniambia niangalie mbele, huku nikiweka suala la masilahi kama kipaumbele."
Anasisitiza kwamba haikuwa kazi rahisi kwake kwa sababu alikuwa akiondoka kwenye radio iliyosababisha asikike Tanzania nzima na kwenda mahali na ndiyo kwanza panachipukia.
"Lakini nikajiuliza, nisingeenda mimi kupakuza Efm, angeenda nani? Nikafikia uamuzi na kuacha kazi Radio One na kujiunga na Efm nilipo mpaka leo na ninaifurahia kazi yangu," anasema.
Familia
Maulid Kitenge kwa kabila ni Mmanyema, pia ni mume wa wake wawili ambao ni Eshe Muhidin na Mwanaidi Yatery, akiwa pia na mtoto mmoja, Shadya Maulid Kitenge anayetajwa kuwa mmoja wa nyota wa mchezo wa tenisi nchini.
©2023 SAN TZ MEDIA
Негізгі бет Ойын-сауық EXCLUSIVE: HISTORIA YA MAULID KITENGE |MMILIKI & MWANZILISHI WA KITENGE TV NA MTANGAZAJI WA MICHEZO
Пікірлер: 2