Fafanuzi rahisi ya kitabu cha UFUNUO WA YOHANA - Sura ya 12 (Na Bishop Dr. Fredrick Simon)
1. MWANAMKE, MTOTO MWANAMUME, NA JOKA 12:1-17
i. Mwanamke
Aya ya 1 “Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua,
na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota
kumi na mbili”.
Mwanamke anayetajwa hapa ni taifa la Israeli. Mara kwa mara, Taifa la Israeli
limekuwa likitajwa kama Mwanamke (Mke wa Mungu).
“Kwa sababu, Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina
lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa
dunia yote.” “ISAYA 54:5
(soma pia - Hosea 2:16).
Jua na mwezi huwakilisha utukufu wa Mungu. Kwa kuwa jua huangaza mchana na
Mwezi usiku, Utukufu wa Mungu utakuwa juu ya taifa hili usiku na mchana, na
nuru itakayoweza kuufikia ulimwengu mzima.
Nyota 12 ni makabila 12 yanayounda taifa hilo.
12:6 Tunasoma: “Yule mwanamke akakimbilia nyikani....”
Waisraeli watakimbilia nyika za Edomu, Moabu na Amoni - 12:6, ISAYA 16: 1-5;
ZABURI 60:9-12. Watakuwa nyikani kwa miaka 3½ - DANIELI 7:25.
Fimbo ya Chuma: Kuchunga kwa fimbo ya chuma humaanisha kumiliki kwa
mamlaka kali. Kama tujuavyo, utawala wa Mungu, sio wa Demokrasia. Ni utawala
mkali, ambapo watu wanapaswa kutii tu bila mjadala wowote. Mungu hana kamati
ya washauri, na hakosei katika maamuzi yake (Kwa kiingereza: Despot).
Yesu atatawala mataifa ZABURI 2:9; UFUNUO WA YOHANA
19:15
Watakatifu wa kipindi cha Agano la Kale watatawala mataifa -
EZEKIELI 34:24; 37:24,25.
Watakatifu wa Agano Jipya watatawala mataifa -
1WAKORINTHO 6:2, 2TIMOTHEO 2:12; UFUNUO WA
YOHANA 2:26,27.
Watakatifu wote watatawala mataifa - ZABURI 149:7-9.
ii. Mtoto mwanamume.12:5 husema, “Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye
atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake
akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.
Wengi hudai ati motto huyu ni Yesu, lakini si kweli. Tunaona mtoto akizaliwa na
mwanamke, ambapo mwanamke huyo ni taifa la Israeli. Hivyo, motto huyo
atajwaye, si mwingine, bali ni wale waisraeli mia arobaini na nne elfu (144,000),
tulioona habari zao katika sura ya saba.
Waisraeli hawa 144,000 watakuwa na mamlaka ya kufanya chochote kwa watu wa
mataifa, na hawataathiriwa na mapigo yatakayokuwa yakiendelea duniani. Hiyo
ndiyo maana hasa ya kuchunga mataifa kwa fimbo ya chuma.
iii. Joka.
12:9 husema, “Yule joka akatipwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi
na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake
wakatupwa pamoja naye.”
Негізгі бет Fafanuzi rahisi ya kitabu cha UFUNUO WA YOHANA - Sura ya 12 (Na Bishop Dr. Fredrick Simon)
Пікірлер: 11