Fafanuzi rahisi ya Kitabu cha Ufunuo wa Yohana - Watakatifu Kipindi Cha Dhiki Kuu (Sura ya 7)
WATAKATIFU WAKATI WA DHIKI KUU - SURA YA 7
Ebu tuone makundi mawili ya watakatifu wanaoonekana wakati wa dhiki kuu.
i. Waisraeli 144,000 - (7:3-8;9;4)
Watu hawa watakaotokea katika makabila 12 ya Israeli, hawatapatwa na madhara ya mapigo ya dhiki kuu - 14:1, kwa sababu wao watakuwa wametiwa muhuri kwenye vipaji vya nyuso zao, muhuri yenyewe itakuwa imeandikwa jina la Mwana Kondoo, na jina la Mungu YEHOVA.
Tunaelewa wazi kwamba, Reuben ni kaka wa Yuda, kwa nini basi Yuda anatajwa kabla ya Reubeni kaka yake katika 7:5?
Zipo sababu kuu 2.
a. Masihi alitokea katika kabila ya Yuda.
b. Reubeni alilala na suria (hawara) wa baba yake, suria aliyeitwa Bilha.
“Ikawa Israeli alipokuwa akikaa katika nchi ile, Reubeni akaenda akalala na Bilha, suria wa babaye, Israeli akasikia habari ....” MWANZO 35:22.
Baba yake akamshusha cheo cha ukubwa.
“3 Reubeni u mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na kwa nguvu.
4 Umeruka mpaka kama maji, basi usiwe na ukuu, kwa sababu ulipanda kitanda cha baba yako, ukakitia unajisi, alikipandia kitanda changu.” MWANZO 39:3-4.
Nafasi hiyo aliipewa Yuda, ambaye tafsiri ya jina lake ni ‘Sifa’, Yuda alikuwa ni mtoto wa nne wa Yakobo (Mwanzo 49:8).
ii. Mkutano mkubwa wa watakatifu - 7:9,13,14
1. Baada ya hayo nikaona, tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao;
“13 Akajibu mmoja wa wale wazee akiniambia, Je! Watu hawa waliovikwa mavazi meupe ni akina nani? Na wametoka wapi? 14 Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe. Akaniambia, Hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.”
Kuna watu wanaodai ati wakati wa dhiki kuu hakuna atakayeokoka, hiyo si kweli! Maandiko hapo juu yanaonyesha wazi kwamba watu wengi wataokolewa wakati wa dhiki kuu; lakini kwa kupata mateso mazito. Watu hawa wataokolewa katika kipindi kigumu mno, mfano wake hauelezeki, ila atakayevumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka. Watu wote hao wataokolewa kutokana na injili itakayohubiriwa na:-
a. Waisraeli 144,000 - 7:3,4
b. Mizeituni miwili (Eliya na Henoko) - 11:3
c. Malaika mwenye injili ya milele (yamkini ni mwinjilisti mkubwa atakayetumiwa kwa kiwango cha juu kuyafikia mataifa) - 14:6,7.
Taifa, kabila, lugha na jamaa, hutajwa pia katika maandiko yafuatayo:- 5:9; 7:9; 11:9; 13:7; 14:6; 17:15.
#bishop #fredricksimon #ufunuowayohana
Негізгі бет Fafanuzi rahisi ya Kitabu cha Ufunuo wa Yohana - Watakatifu Kipindi Cha Dhiki Kuu (Sura ya 7)
Пікірлер: 10