Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akielezea kusikitishwa kwake na namna Mahakama inavyoshughulikia kesi zinazohusiana na ukwepaji wa kodi na ametoa wito kwa mahakama na wadau wake kujipanga kukabiliana na dosari hiyo inayorudisha nyuma juhudi za maendeleo ya nchi.
Mhe. Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 02 Februari, 2017 katika sherehe za uzinduzi wa mwaka wa Mahakama (Siku ya Sheria) zilizofanyika katika uwanja wa Mahakama uliopo Mtaa wa Chimala, Kivukoni Jijini Dar es Salaam na kubainisha kuwa katika kipindi cha kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2016 Serikali haijalipwa kiasi cha Shilingi Trilioni 7.5 licha ya kushinda kesi za ukwepaji kodi zilizokuwa zinawakabili washitakiwa mbalimbali.
Негізгі бет HOTUBA YA RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI KTK SHEREHE ZA UZINDUZI WA MWAKA MPYA WA KIMAHAKAMA mp4
Пікірлер: 3