UWAMINIFU NI NINI?
Uaminifu ni nini? Uaminifu ni tabia ya kuwa mkweli katika kila jambo linalokuhusu wewe au wengine. Kuna wengine sio waaminifu kwao wenyewe na kuna wengine wanashindwa kuwa waaminifu kwa wengine. Uaminifu ni tabia ya kiungu na Mungu mwenyewe anataka na sisi watoto wake tuwe nayo. Mungu ni mwaminifu sana; kwa maana ya kuwa lolote analolosema basi ni sharti alitimilize. Mungu hayupo tayari kuvunja uaminifu wake.
Kati ya wote unaotakiwa kuwaamini bila kuwakatia tamaa ni MUNGU maana sio kigeugeu. Maadamu umekuwa mtoto wa Mungu; Mungu amekupa tabia zake. Kwa sababu wewe ni mtoto wa Mungu basi umebeba tabia za Mungu. Kuna tofauti ya kubeba tabia na kuzidhihirisha(kwa maana ya kuzifanya) hizo tabia. Ni jukumu lako sasa kama mwana wa Mungu kuzidhihirisha tabia za kiungu ulizobeba.
Maandiko yanasema kama alivyo Baba ndivyo tulivyo na sisi. Hivyo kama Baba ni mwaminifu basi na sisi pia ni waaminifu. Tabia hii ya uaminifu kwako je! inaonekana? watu wanaiona? je! wewe ni mwaminifu kwako wewe mwenyewe? ni mwaminifu kwa wengine? ni mwaminifu kwa Mungu? Mmoja ya vitu vinavyosababisha kupandishwa daraja kiroho na kimwili pia ni UAMINIFU. Je! wewe ni mwaminifu katika mambo unayoyafanya? ni mwaminifu katika mazingira unayofanyia kazi? ni mwaminifu kwa wafanyakazi wenzako?
Vivyo hivyo hata kwenye maisha ya imani ili kufikia kiimo na utimilifu wa Kristo ni lazima uwe na uaminifu. Usipokuwa mwaminifu kwenye maisha ya kawaida huwezi kuwa mwaminifu kwenye maisha ya kiroho vilevile usipokuwa mwaminifu kwenye maisha ya kiroho huwezi kuwa mwaminifu kwenye maisha ya kimwili(kawaida). Moja ya tabia ya mtu asiye mwaminifu ni uongo.
Mwanzo 39:1-23
Moja ya vitu vilivyomfanya Yusuph asitawi katika nyumba ya potifa ilikuwa ni uaminifu aliokuwa nao na uaminifu kwa yule aliyemuweka kwenye nyumba yake. Pamoja na kwamba Mungu alikuwa pamoja na Yusuph na alipata kibali machoni pake; kama Yusuph asingekuwa mwaminifu basi asingefika pale alipofika. Mungu anaweza kuwa pamoja nawe,unaweza ukawa umepewa neema, ila ukikosa uaminifu basi huwezi fika unapotakiwa kufika. Kama Yusuph asingekuwa mwaminifu kwenye kazi za ndani alizokuwa anafanya kwa potifa basi asingefika hatua ya kuwa waziri mkuu. Ukiwa mwaminifu haijalishi unakutana na jambo la aina gani; kama jambo hilo sio zuri ni lazima utaepuka tu. Uaminifu ukipungua utajikuta kwenye mambo ya kiMungu unatilia shaka.
Mwanzo 41: 39-41
Wakati mwingine hekima uliyonayo inapimwa na uaminifu ulionao. Mtu mwaminifu anaongozwa na hekima. Ukikutana na mazingira hatarishi hekima itakusababisha ukimbie au kufanya jambo la kuepuka. Kwa sababu ya uaminifu Yusuph alipata neema ya kuwa waziri mkuu wa nchi ; yaani alipata cheo kikubwa zaidi ya kile alichokuwa nacho mwanzo.
Luka 16:10(a), Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia;
Mungu anaweza kukupa mwanzo mdogo; anaangalia kwenye hicho kidogo kama ni mwaminifu. Na kama umekuwa mwaminifu basi anakuamini kwenye yaliyo makubwa.
Je unaitaji kujifunza zaidi piga +255 682 599 376
#ProphetSimonCharisma #charismageneration #kizazikilichokataakufa #kizazikinachoishimilele #tunaishimpakaunyakuo #uzimanamafanikio
CLICK THE "SUBSCRIBE BUTTON" on the bottom right corner of the video.
Follow Us On:
INSTAGRAM: / prophetsimoncharisma
FACEBOOK: / prophetsimoncharisma
#LCM2023 #UzimanaMafanikio #midweekservice
#charismatv #sundayservice #love #prayer #pray #hope #bible #jesuschrist #christian #faith #jesus #motivation #christ
#gospel #meditation #truth #christianity #worship
#believe #holyspirit #spirituality #healing #charismageneration #kizazikilichokataakufa #kizazikinachoishimilele #tunaishimpakaunyakuo #uzimanamafanikio
#scripture #spiritual #grace #loveyourself
#amen #prophetic worship #Haleluya Tv
#prophetic fire #propheticanddeliverance
#propheticandhealingministry
#tanzania #kenya #uganda
Негізгі бет JE UNAWEZAJE! KUWA MWAMINIFU | FAIDA ZA KUWA MWAMINIFU | UWAMINIFU NI NINI?
Пікірлер: 3