"Nilitaka kusema kwamba hizi ni jitihada za serikali kusogeza huduma za afya karibu sana na wananchi. Hospitali kama hizi tulizoea kuzisikia huko Dar es Salaam, Mwanza labda Arusha lakini leo Hospitali hii ipo Katavi, ni maendeleo makubwa sana.
"Nimekwenda kuangalia wodi ya watoto wanaozaliwa kabla ya kutimia. Huduma iliyoko pale ni sawa sawa na huduma nilipokwenda kuangalia Dar es Salaam wodi ya watoto ambao hawakutimia. Mashine za kisasa. Wataalamu wapo. Nimemkuta nesi mzuri sana anawahudumia. Kwa hiyo mambo Katavi ni mazuri mno. Ombi langu kwa Mganga Mkuu, madaktari na watumishi wengine kwenye hospitali hii ni kuendeleza huduma njema, huduma bora kwa wananchi," Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.
Негізгі бет KATAVI NI KAMA DAR ES SALAAM TU-RAIS SAMIA
Пікірлер