Zaidi ya kilometa 250 zinatarajiwa kujengwa katika awamu ya pili ya Mradi wa Uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP), utakaoanza Aprili mwaka huu.
Hayo yameelezwa leo, Alhamisi Januari 18,2024 na Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura) Mkoa wa Dar es Salaam, Geofrey Mkinga wakati akitoa taarifa kuhusu mwenendo wa miradi ya DMDP kwa Kamati ya siasa ya Mkoa na Wilaya zote tano za Dar es Salaam waliotembelea ofisini kwake.
Mkinga amesema awamu ya pili ya DMDP utagharimu zaidi ya Sh1 trilioni fedha zitakazotolewa na Benki ya Dunia (WB) na Serikali ya Uholanzi kwa ajili ya utekelezaji wa miundombinu ya barabara, usimamizi wa taka ngumu (madampo), masoko na vituo vya mabasi, mifereji na bustani.
Негізгі бет Kilometa 250 kujengwa awamu ya pili mradi wa uendelezaji wa jiji la Dar es Salaam (DMDP)
Пікірлер: 4