Mbunge wa Babati mjini Pauline Gekul amesema wananchi wa Mkoa wa Manyara wamekuwa wakihoji kwanini mechi ya finali ya Kombe la Shirikisho la CRDB imeondolewa Mkoani Babati na kupelekwa Uwanja wa New Amaan, Zanzibar.
Gekul amesema kuwa wamewapa maumivu makubwa Wanababati kwa kuwaondolea finali hizo kwa kigezo cha usalama.
Ameiomba Bodi ya Ligi Tanzania na TFF kuangalia upya namna ya kuwapunguzia machungu kwa kuwapa mashindano mengine yatakayochezwa kwenye uwanja wao ulioandaliwa kwa muda mrefu.
Негізгі бет Mbunge ang'aka fainali ya Yanga na Azam kutofanyika Manyara
Пікірлер: 19